Kanisa la Moravian Jimbo la Jamaika

Kanisa la Moravian Jimbo la Jamaika (Jamaica Province of the Moravian Church au kwa jina la kikamili The Moravian Church in Jamaica and the Cayman Islands) ni kitengo cha Kanisa la Moravian duniani. Eneo la jimbo hili ni nchi ya kisiwani ya Jamaika pamoja na funguvisiwa ya Cayman (eneo la ng'ambo la Uingereza) katika Bahari ya Karibi ya Amerika ya Kati. Jimbo hili limeanzisha pia kazi ya misioni huko Kuba.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne